Pages

Monday, July 5, 2010

Rais Kabila wa Kongo atangaza siku mbili za maombolezo

Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo ametangaza siku mbili za maombolezo, baada ya watu 235 kupoteza maisha yao katika moto. Ajali hiyo ilitokea baada ya lori lililopakia mafuta kupinduka

na kuripuka katika Wilaya ya Kivu ya Kusini.



Moto huo, ulienea katika jengo ambako watu walikuwa wakitazama mchezo wa Kombe la Dunia. Watu wengine walikufa walipokuwa wakichota mafuta katika lori hilo. Umoja wa Mataifa pia umesema kuwa wanajeshi wake 5 wa vikosi vya amani walipoteza maisha yao walipokuwa wakiwazuia watu kukaribia lori hilo.

Comments
Add New Search

No comments:

Post a Comment