Pages

Friday, July 2, 2010

Uchaguzi 2010 na Maendeleo ya Kilema

Hello wadau wa maendeleo ya Kilema.

Kama mjuavyo mwaka huu ni mwaka uchaguzi na kila ukipita maeneo ya Tanzania suala kubwa ni juu ya tukio hilo muhimu katika nchi yetu. Wakati mkiendelea kutafakari na kuwaza juu ya uchaguzi huo.. nimeona leo niwaletee swali la Je ni aina gani ya mtu anafaa kuwa Mbunge wetu na Diwani wetu katika Kilema? Jambo hili ni muhimu kwani kama mjuavyo maendeleo yetu yatapatikana tu iwapo tuna uongozi thabiti wenye uelewa wa mambo na ambao unaweza kukabiliana na changamoto za zama tulizopo na sio uongozi unaotaka kuendesha mambo kwa Mazoea.